Wednesday, February 14, 2024

KWANINI NAACHIKA NA KILA MPENZI?

MAPENZI NI NINI?

Mapenzi ni hali ya kuwa na ukaribu wa kihisia kingono kati ya mwanamke na mwanaume. Mvutano wa kihisia kati ya jinsia hizo unaunda mapenzi kila mmoja wao anaanza kujali kuhusu mwingine na kuvutiwa nae kingono.





Jibu: kwanza kama mapenzi ni mvutano wa kihisia pia unaweza kuwa mvunjiko wa kihisia baini ya wapendanao.

Unajua katika hali ya kawaida mapenzi huweza kuvunjika tu, kwasababu huyo mtu ambaye unamahusiano nae mmekutana ukubwani na kutengana inawezekana.

KWA MWANAUME.
1. NAMNA ULIVYO MTONGOZA AU UMEMPATA MWANAMKE WAKO.
Unajua kila mwanaume ana mbinu yake ya kumpata mwanamke ampendae japo kuwa kuwa yawezekana maneno yanaweza kufanana
sasa kwamfano mtu anamtongoza mwanamke wa kujiweka yeye ni tajiri inagli hana kitu, vipi mwanamke akigundua amedanganya hapo kutakuwa na mahusiano kweli? ni wachahche wanaweza kuvumilia lakini wengi wana weza kukimbia.

2. UBAHILI
Mwaname ukiwa bahili sana unaijua fedha wala hauthamini shida za mwenza wako ni rahisi kukimbiwa na mwandani wako akaenda kwa wale ambao wanajua kujitoa hata kwa jambo dogo
Mwanamke anahitaji kupendwa na kujaliwa kwenye kula, kuvaa, kusuka, kupewa vijizawadi hata kama ni kidogo tu.

3. UCHAFU, ULEVI, UHUNI, WIZI, UGOMVI, URAFI, NK
Lazima ujifunze kuwa mtu wa kawaida

Monday, December 11, 2023

KUFAULU KATIKA MAISHA (TO SUCCEEED IN LIFE)

 Mitihani katika maisha ya kila mwanadamu ni jambo ambalo ni la kawaida na ni haki ya kila mmoja wapo anayeishi kwenye huu ulimwengu. Maandiko ya kidini pia hayajamuahidi yeyote kuishi katika raha na starehe bali ni masumbuko mitihani na magumu mpaka siku yake ya mwisho ya kuishi hapa ulimwnguni. 

(Ayu 14:1 SUV

Mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke Siku zake za kuishi si nyingi, naye hujaa taabu)

Mateso

Changamoto ni nyingi sana hata ni ngumu kuzieleza zote baadhi tu ni changamoto zinaweza mkumba binadamu yeyote:

1. Magonjwa ya kudumu au magonjwa ya kupita

2. Kufilisika kiuchumi, kupoteza mali zako, kuibiwa n.k

3. Mapenzi na mahusiano

4. Kukosa ajira, kipato

5. Umasikini

6. Kifo, kufiwa

7. Kufukuzwa kazi

8. Majanga ya asili kama vile mafuriko, matetemeko, vimbunga, magonjwa n.k

9. Kudhurumiwa, kutapeliwa, kudanganywa n.k

10. Ajari n.k


kUFAULU KATIKA MAISHA


Zote hizo ni baadhi ya changamoto ambazo mtu unaweza kukumbana nazo muda wowote katika maisha ya kila siku.


NJIA BORA ZA KUEPUKANA AU KUFAULU KUPAMBANA NA MATATIZO HAYA YA KILA SIKU

1. KUMTEGEMEA MUNGU KWA KILA JAMBO✝✝✝

zipo changamoto nyingi sana mabazo kwa uwezo wetu na akili za kawaida hatuwezi kutatua bali MUNGU pekee ndiye anaweza kuzitatua. kama mwanadamu wa kawaida nadhani tunashuhudia mengi ambayo yako nje ya uwezo wetu (beyond human Nature) hivyo hakuna njia ya kupambana nayo bali ni kusimama na imani zetu na Kuomba MUNGU atuepushie kila lililo nje ya uwezo wetu. mfano Magonjwa mfano mzuri Covid 19, majanga ya asili mfano Tsunami tunashudia nchi za Indonesia, Thailand, India, Sri-Lanka, Malaysia, Myanmar, Bangladesh, Maldives, Reunion Island (French), Seychelles, Madagascar, Mauritius, Somalia, Tanzania, Kenya, Oman, South Africa and Australia

Tsunami

💦

2. KUPAMBANA KWA BIDII NA MAARIFA

inakuhitaji Bidii sana na maarifa ili kupambana na changamoto hizo zilizotajwa

  • kwa kufanya kazi bila kuchagua ili mradi tu inakupatia kipato 
  • kutafuta maarifa mapya kila siku yale yanayoweza kukusaidia katika maisha yako ya kila siku.
  • kusali kwa imani yako kila siku 
  • kufanya mazoezi ya mwili kwaajili ya afya bora
  • kuzingatia lishe bora kwa afya yako
  • kubadili mtindo wa maisha mfanyo kuacha/kupunguza uvutaji wa sigara na matumizi ya madawa ya kulevya, kuacha matumizi ya pombe na vilevi, kupunguza idadi ya wanawake/wanaume unaofanya nao mapenzi
  • kufwata sheria zilizowekwa na jamii au serikali yako ili uishi kwa amani
  • Punguza marafiki wale wasiokuwa na msaada kwako


Saturday, December 3, 2022

UGONJWA WA KUPOOZA (STROKE ) AU KIHARUSI

 Ugonjwa wa kupooza (stroke) au wengine huita ugonjwa wa kiharusi ni aina ya ugonjwa ambao huathiri mfumo wa fahamu na neva za mwili kiujumla. Ugonjwa huu awali ulikuwa unaweza kuwapata watu wenye umri wa juu au makamo lakini kwa  sasa ugonjwa huu unaweza kumpata mtu yeyote yule kuanzia umri wa kati. 

Stroke/kiharusi ni ugonjwa mbaya lakini unamatibau yake ambapo mgonjwa anaweza kutibiwa na akapona japo wengine wanapata ulemavu wa viungo na kuathiri ogani za mwili.



AINA ZA STROKE/KUPOOZA

kuna aina Mbili za ugonjwa huu wa kupooza

1. Ischemic stroke

Aina hii ya stroke hutokana na Mishipa ya damu kushindwa kusukuma damu ndani ya mishipa na kusababisha damu kurundikana na kuganda kwenye mishipa iliyopo kwenye Ubongo wa Binadamu. tukio hili hutokea ghafla kama umeme pale ambapo damu au chembe nyekundu za damu zimerundikana sehemu na kufanya mawasiliano ya baadhi ya mishipa kukata hivyo kusababisha kupooza kwa mwili katika sehemu mbalimbali.

Kama tujuavyo kuwa damu katika mwili ndio husafilisha kila kitu katika mwili wa binadamu ikiwemo mawasiliano na umeme wa mwili kupitia veni za mwili. hivyo damu iikwa ghafla imekatwa katika mishipa iliyopo kwenye ubongo inaweza kusababisha mtu kupooza na kupoteza fahamu.

Sababu za Kutokea Kwa Ischemic Stroke.
i. Mafuta kuganda ndani ya Mishipa ya Damu hivyo kufanya njia iwenembaba sana kusukuma damu kwa wakati na kwa usahihi.

ii. Mishipa kuwa miembaba kutokana na lishe duni au uvutaji wa sigara na pombe katika maisha ya kila siku.

iii. Kutofanya Mazoezi na kuwa na unene uliopindukia kupita kiasi

MADHARA YANAYOWEZA KUTOKANA NA UGONJWA WA AINA HII.
  • - Kupinda mdomo kwa Mgonjwa 
  • -Viungo kukakamaa kama vile mikono, shingo au miguu
  • - Kusinyaa kwenye ubongo kwa baadhi ya wagonjwa
  • - Kupoteza lugha au kuongea
  • - Jicho moja au yote kupoteza kuona au kuona kwa uhafifu
  • -Kupoteza hisia za miguso au kuguswa na kitu huwawezi kuhisi kitu
  • -Kushindwa kutembea au kujongea kutoka sehemu moja kwenda nyingine.
  • -Kupoteza hisia za haja/ kuhisi haja 
  • -Kutosikia vizuri au kutosikia kabisa
  • -Kupoteza kumbukumbu kabisa au kuwa nazo kidogo na mara nyingine kupata ugonjwa wa akili



2. .HEMORRHAGIC STROKE
Aina hii hutokana na Damu kupasua Mishipa ya damu na kuanza kuvuja ndani ya ubongo, mishipa hii midogo sana inayopatikana kwenye ubongo ikianza kuvuja kwenye ubongo inaweza kuganda na kuzuia mawasiliano kwa mgonjwa hivyo kupelekea kupooza.
Aina hii hutokana pale ambapo damu imeshindwa kupita kwenye mishipa ya damu kutokana na msukump mkubwa wa damu hivyo inasababisha mishipa miembaba ndani ya ubongo kupasuka na kumwaga damu kwenye ubongo hivyo kusababisha mtu kupooza


Kwa maelezo zaidi juu ya huu Ugonjwa njoo WhatsApp +255756440628
Nikueleze Tiba na Kinga 
Tiba Vifaa
Tiba Madawa ya asili n.k



Tuesday, September 19, 2017

Namna ya Kufanikiwa katika Biashara zako

Jifunze namna ya kufanikiwa katika biashara zako
Awali ya yote napenda kuwapa salamu zangu ndugu wajasiriamali wote ambao kwa ujumla mnahitaji mafanikio makubwa katika mipango yenu hali kadhalika na maisha kwa ujumla. Katika hali ya kawaida kila mmoja wetu angependa kuona mipango yake ikifanikiwa na kuwa imara kabisa. kufanikiwa  huko ndio njia pekee ya kubadili maisha yako na kuwa miongoni mwa wafanyabiashara wakubwa duniani. ndoto zote hizi za mafanikio huja kwa wale ambao tayari wanataka kubadili mitazamo yao na kuwa chanya badala ya mitazamo hasi. mambo yafuatayo hapo chini yanaweza kuchangia kwa kiasi kikubwa katika mafanikio ya biashara zetu:-


  •  MUDA; Muda ndio kitu cha muhimu zaidi katika mafanikio ya kila mmoja. Biashara yoyote inahitaji uzingatiaji wa muda kama vile muda wa kufungua biashara yako na muda ambao unapaswa kukaa katika biashara yako. wateja wengi wanahitaji kuwa na uhakika na muda ambao biashara yako inakuwa imeanza na kuisha ili kuweza kujenga mazoea na uaminifu katika biashara yako.  Kwa wale wenye biashara za msimu kama biashara za matunda au mazao pia wanahitaji kuzingatia muda kutonana na upatikanaji wa bidhaa zao uli kuteka soko na kupunguza hasara ya kuharibikiwa na bidhaa zao. (kuendana na Muda)
  •  


Saturday, January 21, 2017

JIFUNZE: NAMNA YA KUWA JASIRI/ SHUJAA

Ujasiri ni nini?

Ujasiri ni hali ya kuamua kufanya jambo gumu linaloweza kuwa si rahisi moyo wako au mtu mwingine kuamua kulifanya bali ukajitoa na kulifanya. mfano mtu unaweza kujitoa hata uhai wako ili hali uokoe watu wengine, ukafirisika hata mali zako ilihali uokoe maskini, ukajitosa mahali poote pale bila woga ili hali upate utakacho.

Ujasiri  haupo kwa kila mtu, wapo watu waoga hawawezi hata kujaribu jambo wao hutegemea tu watu wengine ndio maisha yao husonga mbele. Lakini wapo watu ambao hawajali maisha yao wanaweza kufanya lolote hatakama haliwezekani ilimradi waishi maisha mazuri au kupata vitu wavitakavyo kama vile mapenzi, pesa, utajiri n.k 

Ujasiri huja wenyewe pale moyo wako unapoamua jambo bilakipingamizi chochote.. hakuna mtu anayefundishwa ujasiri bali huja wenyewe kutokana na msukumo wa moyo au shinikizo la watu fulani au vitu fulani. "woga ni umaskini" ni kauli ambayo watu wanaojiamini na ni majasiri hutumia katika harakati za kimaisha... mfano unakuta mtu anapenda msichana fulani lakini hawezi kabisa hata kumtamkia anaishia tu kuumia sana na kujihisi kama hana bahati.kumbe ndio kukosa ujasiri kwenyewe.
Sababu za kukosa ujasiri
  1. kutojiamini; unakuta mtu anapenda sana vitu fulani au mtu fulani lakini kutokana na yeye kutojiamin anaweza kuvikosa au kumkosa mtu ampendae.......
  2. kujidharau, kuna baadhi ya watu ujiona wao si mali kitu.. wao wako hadhi ya chini kuliko wengine, au wakajihisi ni wabaya, weusi, waovu sana, hawana akili, maskini kuliko wengine hivyo kujidharau.
  3. Mitazamo hasi; hii ni mitadhamo iwayo akilini mwa watu ambapo mara nyingi watu hujiona kuwa sahihi kimazamo hasa upinzani wa vitu vyenye tija na kushikilia mitazao isiyo kuwa na tija... mfano kunawatu walisha amini kwamba hawawezi kitu kabisa ndio wakajidharau na kuishia kutojiamini.
  4. kukosa msaada/support; moyo wa mtu unaweza kukata tamaa na kutojiamini endapo kwa upande wake hakna anae msimamia wala kumtazama hata kama anafanya jambo la msingi badala yake wakajitokeza watu wanao mbeza au kumkejeli hivyo mtu akaona haina maana kuendelea na jambo alilolitarajia na kujikuta amepoteza ujasiri  n.k
Namna ya kuwa jasiri/ kuwa na ujasiri.
  • kujiamini; hakuna binadamu aliye kamilika, kama umeamua kufanya jambo lolote lenye msaada katika maisha yako au a wengine.. jiamini ujioe hata kama watu watakushangaa, au kukucheka, kukubeza kukukejeli n.k .... "uoga ni umaskini"
  • Simama imara mwenyewe; daima usitetereke kwa yale ambayo watu wanakunenea bali simama imara na sikuzote usingoje shukurani ... songa mbele
  • kuwa na tazamo chanya, ukiwa na mtazamo hasi daima hauwezi kufanikiwa bali jitahidi kuwa na mtazamo chanya ili mambo yako yawe chanya na itakusaidia kuwa jasiri sana

Monday, July 13, 2015

Heshimu hisia zako

Onesha upendo kwenye music kama ukuoneshavyo wewe unapokuwa umekosa peace of mind na ma stress ya kutosha, music hufungua mishipa ya damu iliyo zibwa kwa majonzi na kukufanya ufikirie vizuri na kuwa na amani ya kutosha. Sometime unaweza ukawa mtu uliyekata tamaa lakini music hutia moyo na kukufanya uwe na nguvu mpya tazama mfano wanajeshi katika mambo yao lazima watatia hata music kidogo kutiana moyo si unafeel so cool unapokuwa umetulia home na washikaji unakula masong ya kumwagaa show love hisia zako

KWANINI NAACHIKA NA KILA MPENZI?

MAPENZI NI NINI? Mapenzi ni hali ya kuwa na ukaribu wa kihisia kingono kati ya mwanamke na mwanaume. Mvutano wa kihisia kati ya jinsia hizo ...